Millionaire  Ads

simba vs Azam ni vita ya dakika 90


Michezo matatu ligi kuu Tanzania bara vpl kupigwa leo katika mikoa mitatu tofauti
Jijini Dar es Salaam
 simba wataonyeshana ubabe na wanalambalamba Azam fc katika mchezo ambao utakuwa ni mgumu na utabiri wake hauelezeki,



Azam ambao raundi ya pili wamekifanyia maboresho makubwa kikosi chao kuanzia benchi la ufundi mpaka wachezaji.

Simba wanaingia Uwanja wa taifa wakiwa na kumbukumbu ya kichapo cha goli moja toka kwa Azam siku chache zilizopita katika mchezo wa finali kombe la mapinduzi.

Tutarajie soka safi na lenye ushindani ikizingatiwa simba inatafuta taji la vpl ambalo imeliasi kwa mudda mrefu wakati azam ikijaribu kurejea katika nafasi ya tatu.

 Jijini Mbeya
Kutakuwa na derby ya mkoa huo ambapo wajelajela Tanzania Prisons watakipiga na ndugu zao wa Mbeya city.


Mkoani Mtwara
Ndanda wao watawakaribisha jiranizao Majimaji toka mjini songea katika mchezo ambao utakuwa mkali hasa ukifutilia Matokeo mabovu kwa timu hizi mbili msimu huu.


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "simba vs Azam ni vita ya dakika 90"

Back To Top