Millionaire  Ads

Mali 0 - 0 Tanzania, AFCONU17 Gabon, Serengeti wazidi kuweka rekodi Afrika




Serengeti boys waanza na sare na bingwa mtetezi Afcon U17 Gabon
Timu ya Taifa ya Tanzania chini ya umri wa miaka 17 Serengeti Boys leo imegawana pointi na bingwa mtetezi wa michuano hiyo timu ya taifa ya Mali.
Mali walionekana wazuri zaidi kipindi cha kwanza na kuutawala mchezo kwa asilimia kubwa huku Serengeti Boys wakifanya kazi kubwa kulinda goli lisiingie.
Kipindi cha pili Serengeti Boys waligeuza mchezo na kuwaduwazaa mali na kushindwa kuamini kuwa Serengeti ndio wale wa kipindi cha kwanza au wengine, waliutawala mpira vizuri hasa eneo la kati ambapo kiungo Kelvin Naftal alifanya anavyotaka.
Hadi mwisho wa mchezo wenyeji Mali 0 – 0 Tanzania.
Hii inamaana kuwa Tanzania wanahitaji ushindi katika timu zilizosalia ili waweze kufuzu kwa kombe la dunia nchini India.

Kilalakheri Tanzania kilalakheri Serengeti Boys.

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comment untuk "Mali 0 - 0 Tanzania, AFCONU17 Gabon, Serengeti wazidi kuweka rekodi Afrika"

Back To Top