Millionaire  Ads

Ajib rasmi yanga miaka miwili,kaburu asita kutoa majibu


Mshambuliaji hatari wa Simba na timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Ibrahim Ajib Migomba amesaini kandarasi ya miaka miwili kuitumikia timu ya Yanga.
Hayo yalinukuliwa na waandishi wa habari baada ya kukihoji Chanzo cha ndani cha timu ya Yanga ambacho kilikiri kumpa mkataba mchezaji huyo.
Akihojiwa na EFM radio ya jijini Dar es salaam jana alhamisi june 15, Kaburu alisita kukubali au kukanusha taarifa hizo kwa kudai kuwa wakuulizwa na mchezaji husika ndie anaejua ukweli ulivyo “sisi tumempa ofa yetu hajasaini na Simba inautaratibu wake hatuwezi kumlazimisha mchezaji” alisema Kaburu, “ukitakata kujua kama kasaini yanga muulize mwenyewe atakuwa na majibu” Kaburu aliongeza.

Alipoulizwa katibu mkuu wa Yanga Mkwasa yeye alisema wao wapo kimya kimya taarifa zitawajia punde na kuhusu ukata ndani ya kilabu hiyo alisisitiza kuwa timu sasa ipo vizuri na haina ukata tena.
Inasadikiwa katika mkataba wa Ajib amepewa nyumba na gari la kutembelea.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Ajib rasmi yanga miaka miwili,kaburu asita kutoa majibu"

Back To Top