Millionaire  Ads

Ronaldo aendelea kuweka rekodi Ulaya goli mbili ni rekodi mpya kwake, ampiku Messi kimaajabu


Ronaldo aendelea kuweka rekodi Ulaya goli mbili ni rekodi mpya kwake
Licha ya kutwaa kiatu cha dhahabu katika mazingira ambayo Hakuna alitegemea CR7 jana aliingia kwenye kitabu cha kumbukumbu cha wachezaji wachache waliofunga magoli mawili katika mchezo wa fainali wa kombe hilo akiungana na  Daniele Massaro (Milan 1994), Karl-Heinz Riedle (Borussia Dortmund 1997), Hernán Crespo (Milan 2005), Filippo Inzaghi (Milan 2007) and Diego Milito (Internazionale 2010).
Ikumbukwe kuwa Hakuna mchezaji yoyote ambae amewahi kufunga goli tatu katika mchezo wa fainali.
CR7 jana aliisaidia Real Madrid kutwaa kikombe cha pili mfululizo katika michuano ya ligi ya mabingwa Ulaya baada ya kufunga magoli mawili na mawili wakigawana  Casemiro na Marco Asensio.
Ronaldo licha ya kutwaa kiatu cha dhahabu yeye ndie mfungaji mwenye magoli mengi kwa msimu mmoja alifanya hivyo msimu wa 2014/15 alifunga goli 17.
CR7 ndie mwenye rekodi ya kufunga magoli mengi katika hatua ya makundi alifunga goli 11 msimu wa 2014/15. Messi anafuata kwa kufunga goli 10 katika makundi.

CR7 ndie anaeongoza kuwa na magoli mengi katika historia ya ligi ya mabingwa amefunga magoli 105 baada ya kucheza michezo 140 akifuatiwa na messi mwenye magoli 94 baada ya kucheza michezo 115.





Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Ronaldo aendelea kuweka rekodi Ulaya goli mbili ni rekodi mpya kwake, ampiku Messi kimaajabu"

Back To Top