Millionaire  Ads

MALINZI, MWESIGWA MAMBO MAGUMU WARUDISHWA TENA RUMANDE



Rais wa shirikisho la miguu nchini Tanzania Jamali Malinzi na katibu wake Celestine Mwesigwa Pamoja na mhasibu wa TFF Isinde Isawafo Mwanga kwa mara ya pili leo wamerudishwa tena lupango  baada ya ushahidi unaowakabili kutokamilika.
Watatu hao leo walipandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yao katika mahakama yahakimu mkazi Kisutu.
Baada ya kusomewa mashitaka yao kesi yao imepelekwa mbele hadi july 30 mwaka huu itakapotajwa tena.
Wamesomewa mashitaka 28 ya kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF iliyopo katika banki ya Stanbic, Dar es Salaam.
Malinzi aliingia madarakani 2013 baada ya kumshinda mpinzani wake Athumani Nyamlani.
Uchaguzi huu haumhusu Malinzi tena baada ya kukosa sifa za kugombea Kutokana na kutofanyiwa ‘interview’

Uchaguzi mkuu utafanyika August 12 mwaka huukatikati ya nchi Dodoma

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "MALINZI, MWESIGWA MAMBO MAGUMU WARUDISHWA TENA RUMANDE"

Back To Top