Millionaire  Ads

MRITHI WA MAYANJA HADHARANI NI MASOUD DJUMA RAIA WA BURUNDI


Hatimae kitendawili cha nani kuirithi mikoba ya Mayanja ndani ya Simba Sc kimeshatatuliwa baada ya kumpa mkataba mrudi Masuod Juma ambae alikuwa anakinoa kikosi cha Rayon Sports.
Akizungumza na waandishi wa habari msemaji wa timu ya Simba Haji Manara amesema “Juma ni mzoefu wa soka la Afrika kwa kucheza na kufundisha” aliendelea kusema “wakati wa uchezaji wake walishawahi kucheza na mtanzania Peter Manyika ”.

Kocha huyo anasifika kwa soka la nguvu na kasi ametua leo jijini Dar es salaam na ametambulishwa rasmi mbele ya waandishi wa habari.
Wasifu wa kocha:
Djuma Masoud (alizaliwa Agosti 30, 1977) amezichezea klabu za Prince Louis (2002), Rayon Sport (2003-2009) na Inter Star (2010). 

Pia, Manara alimtambulisha meneja mpya wa klabu hiyo, Richard Robert ambaye anachukua nafasi ya Cosmas Kapinga aliyerejea kwa mwajiri wake kuendelea na kazi yake ya udaktari.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "MRITHI WA MAYANJA HADHARANI NI MASOUD DJUMA RAIA WA BURUNDI"

Back To Top