Millionaire  Ads

CHRISTIANO RONALDO ASAINI MIAKA MITANO MADRID


Siku ya jumatatu mchezaji mwenye thamani kubwa Duniani amesaini mkataba wa kuitumikia Real Madrid kwa kipindi kingine cha miaka 5,
mkataba ambao utamfanya awe ndie mchezaji anaelipwa pesa nyingi zaidi $88m (80 million euros, £71 million) kwa mujibu wa American magazine Forbes.
“Ninachokitaka ni kuendelea kufurahia miaka iliyosalia kucheza, Nna miaka kumi (10) mbele ya kucheza”ni maneno ya Ronaldo baada ya kusaini mkataba huo.
“mwaka huu ndio mwaka niliokuwa nauwaza kiukweli nimetimiza ndoto zangu nimeshinda mataji mawili taji la ulaya, mabingwa ulaya na kusaini mkata huu”
Ronaldo mwenye goli 371 katika mechi 360 tangu ajiunge na Real Madrid 2009, pia amefanikiwa kuchukua kombe la ligi ya mabingwa mara mbili,taji moja la laliga na mataji mawili ya kombe la ligi.

Wachezaji wengine wanategemewa kusaini mikataba na miamba hiyo ya soka ni Gareth Bale, Luka Modric na Toni Kroos
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "CHRISTIANO RONALDO ASAINI MIAKA MITANO MADRID"

Back To Top