Millionaire  Ads

BARCELONA 6 - 1 PSG, historia yaandikwa ligi ya mabingwa Ulaya



Maajabu ya soka yametokea jana usiku baada ya PSG kukubali kipigo kitakatifu cha goli 6 – 1 nyumbani kwa Barcelona.

PSG walihitaji sare au kufungwa goli zisizozidi tatu ili kuweza kutinga hatua ya roba fainali ya ligi ya mabingwa Kutokana na ushindi walioupata February 14, wa goli 4 – 0.

Mchezo wa jana ulianza kwa wenyeji kujipatia goli ndani ya dakika tatu lililofungwa na Luis Suarez baada ya mlinzi wa PSG Marquinhos kukosea kuokoa mpira uliopigwa na Rafinha na kutua kwenye kichwa cha Suarez.


Dakika ya 40 Layvin Kurzawa alijikuta akiipatia Barcelona goli la pili akiwa anajaribu kuokoa mpira ulipigwa Kuelekea golini na Andres Iniesta,

Mpaka mapumziko Barcelona 2 – 0 PSG

Dakika 48 Thomas Meunier alimkwatua Neymar na mwamuzi wa mchezo huo aliamuru ipigwe penati, penati ilipigwa na Lionel Messi na kuipatia timu yake goli la 3.


Mpira uliochongwa na Marco Verratti ulitua kichwani mwa Layvin Kurzawa nae aliuunganisha hadi kwa Edson Cavani ambae aliipatia PSG goli mnamo dakika ya 62.

88’ Neymar alifunga kwa uhodari mkubwa adhabu ya moja kwa moja na kuipatia Barca goli la 4, dakika 2 badae Marquinhos alimfanyia madhambi Suarez kwenye eneo la penati na kuamuriwa ipigwe penati ambayo ilifungwa tena na Neymar na kuipa timu yake goli la 5.


Dakika 90+5 Sergi Roberto scores aliibuka shujaa wa mchezo baada ya kuipatia Barca goli muhimu sana na la kukumbukwa kufuatia kazi nzuri iliyofanywa na Neymar.



Hadi mwisho wa mchezo Barcelona  6 – 1 PSG, hivyo Barcelona wamesonga mbele kwa jumla ya magoli 6 – 5.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "BARCELONA 6 - 1 PSG, historia yaandikwa ligi ya mabingwa Ulaya"

Back To Top