Millionaire  Ads

Matokeo, Ratiba na Msimamo wa ligi kuu ya England, Arsenal hali tete, Leicester waendelea kujiimarisha, Everton waipiku Man U



Timu ya Everton jana rasmi imeweza kuitoa Manchester United katika nafasi yake ya 6 ambayo imedumu nayo kwa muda mrefu sana.
Ushindi wa Everton wa goli 4 kwa  0 dhidi ya Hull City umeifanya Everton kufikisha pointi 50 sawasawa na Arsenal angalia Msimamo upo chini na kukaa katika nafasi ya 6.

Everton wamecheza michezo mitatu zaidi ya Manchester United na miwili zaidi ya Arsenal na kutumia michezo hiyo kuipiku United na kuikuta Arsenal.
Ushindi huo ambao ulitokana na magoli mawili ya Romelu Lukaku ndani ya dakika 1 na Dominic Calvert-Lewin 9’ na Enner Valencia 78’.

Wakati huohuo timu ya Arsenal imekubali kipigo cha goli 3 – 1 dhidi ya  West Bromwich Albion katika mchezo wa mapema jana.
Matokeo hayo yameamsha upia Msimamo wa mashabiki wakutaka  kocha wao Arsenal Wenger afukuzwe kwa kuwa ameshindwa kufanya kile wadau wanapenda.


Matokeo yote ya jana ni kama ifuatavyo:
West Bromwich Albion 3 - 1 Arsenal
Stoke City 1 - 2 Chelsea

West Ham United 2 - 3 Leicester City

Crystal Palace 1 - 0 Watford
Everton 4 - 0 Hull City
Sunderland 0 - 0 Burnley

AFC Bournemouth 2 - 0 Swansea City

Michezo ya leo jumapili
Middlesbrough VS Manchester United  15:00
Tottenham Hotspur VS Southampton  17:15
Manchester City VS Liverpool 19:30

Msimamo wa EPL baada ya michezo ya jana


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Matokeo, Ratiba na Msimamo wa ligi kuu ya England, Arsenal hali tete, Leicester waendelea kujiimarisha, Everton waipiku Man U"

Back To Top