Millionaire  Ads

Stars mguu sawa kuivaa Botswana, TFF yapunguza viingilio


Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars leo inaikaribisha timu ya Taifa ya Botswana katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa ambao upo katika kalenda ya FIFA.
Wachezaji wanaocheza soka nje nchi wameitwa ili kuhakikisha timu yetu inapata Matokeo chanya ili ipate alama katika shirikisho la mpira wa miguu duniani na shirikisho la mpira wa miguu Afrika ambapo Tanzania ipo chini sana ukilinganisha na Botswana.
Mchezaji kiongozi wa timu hiyo Mtanzania anaekipiga huko ubeligiji katika timu ya Genk amerekodiwa na vyombo vya habari akisema  yafuatayo Kuelekea katika mchezo huo
“Ni kweli katika timu ya taifa kunahitajika uzoefu lakini ukiangalia kwa muda ambao Tanzania imekuwa ikishiriki mashindano nafikiri bado hatujakuwa katika nafasi nzuri pamoja na kuwa tulikuwa na wachezaji wazoefu lakini bado hatukuweza kufanikiwa kwa vile tulivyokuwa tunataka tumpe nafasi kocha ya kufanya anachotaka”
Kocha wa timu ya Taifa Mayanga amesema anaamini timu yake itafanya vizuri katika mchezo wa leo.
Viingilio vimepunguzwa ili watanzania wote wenye nia ya kuuona mchezo huo waweze kujitokeza kuipa hamasa timu yao.
Viingilio ni kama vifuatavyo:
Mzunguko sh 3000 badala ya sh 5000/=
VIP A sh 15,000/=
VIP B na C sh 10,000/=


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Stars mguu sawa kuivaa Botswana, TFF yapunguza viingilio"

Back To Top