Millionaire  Ads

Daniel Sturridge na Adam Lallana ‘fit’ kuwavaa Watford leo jumatatu,


kama una tangazo lako tafadhali tuwasiliane ili tukutangazie kwa bei nafuu kabisa, DMrutu ni kwa ajili ya watu wote, karibuni sana


Leo usiku majira ya saa nne usiku majogoo wa London timu ya Liverpool itakuwa ugenini kutafuta alama tatu muhimu na kuendelea kujikita katika nafasi ya nne ambapo jana timu za jiji la Manchester zilishindwa kuindosha Liverpool baada ya kukubali kupoteza alama mbili kila timu.

Lallana amefanya mazoezi na kikosi cha kwanza baada ya kukaa nje kwa muda wa mwezi mmoja Kutokana na majeruhi yaliyokuwa yanamkabili.
Kwa sasa Liverpool na Manchester City wanapointi sawa 66ila Liverpool inauwiano mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa katika michezo 34.

Wakati Liverpool wakifurahia kurudi kwa Lallana na Daniel Sturridge Watford wao watakosa huduma ya beki wao Craig Cathcart ambae ana matatizo ya nyonga, pia itawakosa Younes Kaboul, Roberto Pereyra na mshambuliaji wao Mauro Zarate.

Kwa upande wa Liverpool itawakosa Jordan Henderson, Sadio Mane, Ragnar Klavan na Danny Ings.

Kocha wa Liverpool amenukuliwa na SKY Sport akisema anaiamini timu yake na kila mmoja kwenye timu yake anania ya kubaki nne bora ‘BIG 4’
                                                  
kama una tangazo lako tafadhali tuwasiliane ili tukutangazie kwa bei nafuu kabisa, DMrutu ni kwa ajili ya watu wote, karibuni sana




Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comment untuk "Daniel Sturridge na Adam Lallana ‘fit’ kuwavaa Watford leo jumatatu,"

Back To Top