Millionaire  Ads

Ghana vs Gabon, Kocha wa timu ya taifa ya Ghana U17 (Black Starlets) Paa Kwesi Fabin ameapa kutoionea huruma Gabon katika mchezo wake wa leo.


Baada ya kutoa kipigo kizito kwa mabingwa wa Africa chini ya miaka 17 wa mwaka 2003 cha goli 4 – 0 kocha Paa Kwesi Fabin amesema anachoangalia yeye ni ushindi tu kwa kila timu atakayokutana nayo na sivinginevyo aliiambia CAFonline.
mchezo huo utapigwa saa mbili nusu kwa saa za afrika mashariki.
Timu ya Gabon ndiyo mwenyeji wa michuano ya mwaka huu lakini katika mchezo wake wa kwanza ilikubali kichapo cha goli 5 – 1 kutoka kwa timu ya Taifa ya Guinea U17.
Mchezo wa leo Gabon watakuwa wanahitaji ushindi kwa njia yoyote ili kujisafishia njia ya kucheza nusu fainali, wakati Ghana wao wakishinda leo tayari watakuwa washatinga katika hatua ya nusu fainali.
Timu zitakazofika hatua ya nusufainali zote zitapata tiketi ya kucheza kombe la dunia nchini india badae mwaka huu.

Ratiba ya leo na Msimamo wa kundi A, angalia chini hapo:



Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comment untuk "Ghana vs Gabon, Kocha wa timu ya taifa ya Ghana U17 (Black Starlets) Paa Kwesi Fabin ameapa kutoionea huruma Gabon katika mchezo wake wa leo."

Back To Top