Millionaire  Ads

Hesabu za Arsene Wenger zimebaki kwa Liverpool pekee


Unaweza kusema mzee Wenger atacheza michezo miwili katika siku moja nikimainisha atacheza mchezo wake huku akiomba Liverpool itoke sare au ifungwe ili yeye na timu yake waingie katika nafasi ya 4 ili kuweza kupata nafasi ya kushiriki ligi ya mabingwa hatua ya mtoano.
Jana usiku Arsenal walipata ushindi wa goli 2 – 0 dhidi ya Sunderland
Ila kwa timu itakayoshika nafasi ya nne itabidi tena iombe dua mbaya kwa Manchester United ifungwe katika Fainali ya Europa ili nafasi ya nne iwe salama kinyume cha hapo itabidi timu itakayoshika nafasi ya nne ishiriki Europa.
Manchester City yenyewe ni imejihakikishia kushika nafasi ya tatu au ya nne baada ya jana kuishindilia timu ya West Bromwich Albion kwa goli 3 – 1 na kujisfikishia jumla pointi 75 ambazo Arsenal anaweza kufika ila City anauwiano mkubwa sana wa goli ya kufunga na kufungwa 36, wakati Arsenal ina uwiano wa magoli 31, ili Arsena iweze kuitoa City kwenye nafasi yake anahitajika ashinde goli zisizopungua 6 huku akiiombea City ipoteze.

Hivyo tunaweza kusema Hesabu za Wenger zimesalia kwa Liverpool pekee.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comment untuk " Hesabu za Arsene Wenger zimebaki kwa Liverpool pekee"

Back To Top