Millionaire  Ads

Real Madrid wakishinda jumapili Malaga kulamba €1,Messi 98% mfungaji bora Laliga





Endapo Real Madrid watashinda au watatoa sare mchezo wao wa mwisho wa ligi kuu ya Hispania dhidi ya Malaga watakuwa wametwaa kome la ligi hiyo hvyo basi kwa mujibu wa mkataba kipindi cha manunuzi ya mchezaji  Isco toka Malaga kwenda Real Madrid kinasema endapo Isco ataisadia timu ya Madrid kutwaa ubngwa wa Laliga basi Madrid watalipa €1.
Isco alisajiliwa na Real Madrid mwaka 2013 kwa kiasi cha €27m, katika usajili huo kuna kipengele ambacho kinasema endapo Madrid watatwaa kombe ndani ya miaka mitano ya ligi basi itabidi wailipe Malaga  €1.
Real Madrid inahitaji sare au Matokeo mabaya kwa Barcelona ili iweze kutwaa ubingwa wa Laliga.
Real Madrid wana pointi 90 katika michezo 37 wakati Barcelona wao wana pointi 87 katika michezo 37.
Wakati huo huo mshambuliaji wa Barcelona Lionel Messi 98% ndio atanyakua kiatu cha mfungaji bora wa ligi  kuu ya Hispania.

Messi amefunga magoli 35 msimu huu katika michezo 33aliyocheza, huku akiwaacha mbali Suarez mwenye goli 28 katika michezo 34 na Ronaldo mwenye goli 24 katika michezo 28.

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comment untuk "Real Madrid wakishinda jumapili Malaga kulamba €1,Messi 98% mfungaji bora Laliga"

Back To Top