Millionaire  Ads

Claudio Bravo aivusha Chile mbele ya Ureno, adaka penati 3 mfululizo


Golikipa wa timu ya Taifa ya Chile ambae pia ndie mlinda mlango wa timu ya Manchester City ya England jana usiku aliibuka shujaa wa mchezo wa nusu fainali baada ya kuipeleka timu yake ya Chile Fainali ya kombe la Mabara.

Mchezo wa jana ulikuwa mgumu kwa kila upande na kupelekea dakika 90 kuisha bila goli lolote kwa kila timu.

Dakika 120 pia ziliisha bila timu yoyote kupata goli, na ndipo sheria ya mikwaju ya penati ilipoamuliwa na kupigwa.

Ushujaa wa Bravo ulionekana muda huu wa penati baada ya kuondoa mikwaju mitatu ya mwanzo ya Ureno huku Chile wakipata mikwaju yote ya mwanzo.

Bravo aliokoa mikwaju ya Ricardo Quaresma, Moutinho na Nanj huku chile wakifunga kupitia kwa Vidal,Sanchez na Aranguiz.


Kwa mantiki hii Chile wametinga fainali ya michuano hii wakimsubiri mshindi katika mchezo wa leo kati ya Ujerumani na Mexico.


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Claudio Bravo aivusha Chile mbele ya Ureno, adaka penati 3 mfululizo"

Back To Top