Millionaire  Ads

K.V. Oostende 3 – 1 K.R.C GENK, Ndoto ya Samatta kucheza michuano ya Ulaya yaota mbawa.videomagoli yote zipo





Rasmi timu ya Genk anayokipiga mtanzania Mbwana Ali Samatta haitakuwepo tena kwenye mashindano makubwa ya Ulaya baada ya jana kukubali kichapo cha 3 - 1 kutoka kwa Oostende katika mchezo wa mwisho ambao ndio ulikuwa unaamua timu ya kwenda Europa ligi hatua ya mtoani.
mchezo huo uliopigwa katika dimba la Versluys Arena, Ostend. Magoli ya Oostende yalifungwa na Akpala  27',Rozehnal 32' na Jali 51' wakati goli la Genk likifungwa na Schrijvers 45' kwa mkwaju wa penati penati baada ya Ruslan Malinovsky kukwatuliwa eneo la hatari.

Timu ya Genk ilifika hatua hiyo baada ya kufunga timu ya Sint-Truiden V.V. katika mchezo wa nusu fainali ya playoff ya kuwania kufuzu kwa hatua ya mtoano ya Europa league kwa goli 3 – 0 ambapo Samatta alifunga goli la tatu.
katika mchezo wa jana Samatta alicheza dakika zote 90


Kwa Matokeo hayo ya jana Genk itabidi isubiri msimu wa 2018/19 huenda wakapata nafasi ya kurudi michuano mikubwa ya Ulaya.
video magoli yote ya mchezo huo >>>

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "K.V. Oostende 3 – 1 K.R.C GENK, Ndoto ya Samatta kucheza michuano ya Ulaya yaota mbawa.videomagoli yote zipo"

Back To Top