Millionaire  Ads

South Africa vs Tanzania 18:00,jumapili july 2, 2017 Mtoto hatumwi dukani kesho



Kesho jumapili july 2, 2017 Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars inashuka Dimbani kuwania kutinga nusu fainali ya COSAFA dhidi ya wenyeji wao Afrika Kusini, mchezo utakaoanza saa 12 jioni kwa saa za Tanzania.
Stars imeingia Robofainali baada ya kuongoza kundi kwa kujikusanyia jumla ya Pointi 5, na kuziacha timu za Angola, Mauritius na Malawi zikirudi makwao.
Mchezo wa kesho ni kipimo tosha kwa Stars Kuelekea kwenye mchezo wake wa kuwania kucheza fainali za Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani ‘CHAN’ dhidi ya Rwanda 12/07/2017.
Wachezaji wa Tanzania wanaendelea kuimarika siku hadi siku na kuanza kuleta matumaini kwa wapenda soka wa Tanzania ambao wamekata tama na timu yao ya Taifa kwani kwa miaka nenda rudi inasindikiza.
Huenda huu ukawa mwanzo mzuri kwa soka letu, watanzania tuungane kuipa sapoti timu yetu ya Taifa huenda wachezaji wakajituma ipasavyo na kuiletea sifa nchi yetu.
Faida za COSAFA zipo nyingi kwa wachezaji wetu ikumbukwe hiki ni kipindi cha usajili, jitihada za wachezaji ndio neema kwa taifa letu, huenda tukauza baadhi ya nyota wa timu ya yetu ya Taifa kwenda kwenye vilabu vikubwa Afrika.
Mchezo mwingine utakuwa baina ya Swaziland vs Zimbabwe saa 20:30


Kilalakheri Tanzania hapo kesho mkumbuke mamilioni ya Watanzania tupo nyuma yenu.

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "South Africa vs Tanzania 18:00,jumapili july 2, 2017 Mtoto hatumwi dukani kesho"

Back To Top