Millionaire  Ads

Uongozi wa simba kukutana leo kujadili mustakabali wa viongozi wao na kupitia katiba


Ilikuwa Alhamisi Juni 29, 2017 Rais wa timu ya Simba ndugu Evans Aveva na makamu wake ndugu Geoffrey E,Nyange alimaarufu ‘Kaburu’ walipandishwa mahakamani kusomewa mashtaka yanayowakabili.
Viongozi hao walisomewa mashtaka matano ikiwemo kughushi nyaraka, kutakatisha fedha nk.
Aliekuwa kiongozi wa Simba kwa kipindi cha nyuma Ismail Adden Rage alitoa ufafanuzi juu ya mstakabali wa Simba endapo viongozi wanapatikana na jambo zito kama hilo kwa mujibu wa Katiba ya Simba.
Ismail Adden Rage alisema “kitakachoendelea ni kuitisha mkutano mkuu na kumchagua kiongozi ambae amehudumu kwa muda mrefu ndani ya kilab ‘Senior’ ndie atapewa jukumu la kuiongoza timu”.
Katiba hiyo inaonya kama viongozi watatiwa hatiani basi watakuwa wamepoteza sifa za kuiongoza Simba.
“Huruhusiwi tena kuwa kiongozi katika klabu yoyote ile, vilabu vya mpira vyote vimesajiliwa kwa msajili wa vyama vya michezo, mimi binafsi nimewahi kupata matatizo lakini kwa bahati nzuri mahakama ya rufaa ilinisafisha. Kwa kuwa mahakama ya rufaa ilinisafisha, basi kwa maana hiyo katika maisha yangu bado sijawahi kutiwa doa mahali popote.”

“Kwa bahati mbaya ikitokea wakatiwa hatiani, lazima wakate rufaa waombe kusafishwa lakini kama wenyewe wataridhikabasi hawawezi kuwa viongozi tena wa michezo kwa sababu sheria za nchi wala katiba ya Simba haziruhusu.”Alisema Rage

Leo jumamosi mkutano umeitishwa kwa lengo la kujadili na kujua mustakabali wa timu ya Simba barua inajieleza hapo chini

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Uongozi wa simba kukutana leo kujadili mustakabali wa viongozi wao na kupitia katiba"

Back To Top