Millionaire  Ads

Ujerumani 3 – 1 Cameroon, Ujerumani yatinga Nusu fainali kombe la Mabara.



Mabingwa wa Afrika Timu ya taifa ya Cameroon imeondoshwa rasmi katika michuano ya kombe la Mabara baada ya kupokea kipigo cha goli 3 – 1 toka kwa mabingwa wa Dunia timu ya taifa ya Ujerumani.
Magoli yote manne yamefungwa kipindi cha pili, Ujerumani ndio walianza kufungua ukurasa wa magoli mnamo dakika ya 48 pale




Kerem Demirbay alipopiga shuti upande wa kushoto mwa kipa na kumuacha kipa wa Cameroon akiuangalia tu.
Dakika ya 64 ya mchezo mchezaji Ernest Mabouka wa Cameroon alipewa kadi nyekundu Kutokana na mchezo mbaya alioucheza.
Dakika 67 na 82 Ujerumani walipata goli la pili na la tatu kupitia kwa Timo Werner, 

huku lile la kufutia machozi la Cameroon likifungwa na
Vincent Aboubakar dakika ya 79.

Kwa Matokeo hayo timu za Cameroon na Australia zinarudi makwao na kuziacha Ujerumani na Chile zikienda Nusu fainali.
Cameroon wameaga mashindano wakiwa wa mwisho katika kundi B kwa kuambulia pointi 1 tu, wakati Australia wao wakiwa na pointi 2.
Ujerumani ndio kinara wa kundi B kwa kujikusanyia pointi 7 wakati Chile wanapointi 5 .
Nusu fainali ya kwanza itakuwa tarehe 28/06/2017 kati ya Portugal vs Chile
Nusu fainali ya pili itchezwa Tarehe 29/06/2017 kati ya Germany vs Mexico


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Ujerumani 3 – 1 Cameroon, Ujerumani yatinga Nusu fainali kombe la Mabara."

Back To Top