Millionaire  Ads

ELCLASSICO KUPIGWA BILA RONALDO NCHINI MAREKANI, UCHAMBUZI NA UTABIRI





Mabingwa wa UEFA Champions league timu ya Real Madrid watakutana na vinara wa wa kombe la vilab la kimataifa ICC timu ya Barcelona katika Elclassico ya kwanza tangu kumalizika kwa msimu wa 2016/17.
Real Madrid wanakutana na Barca bila nyota wake C. Ronaldo ambae alipewa mapumziko kufuatia kuitumikia timu yake ya taifa ya Ureno katika michuano ya kombe la mabara.
Tukiangalia timu ya Real Madrid:
Wachezaji ambao wapo na timu nchini marekani ni
Makipa:  Navas, Casilla, Yanez, L. Zidane
Mabeki: Carvajal, Ramos, Varane, Nacho, Marcelo, Theo, Quezada, Tejero, Achraf, Manu
Viungo: Kroos, Casemiro, Modric, Isco, Ceballos, Kovacic, Oscar, Franchu
Washambuliaji: Benzema, Bale, Vazquez, Gomez, Mayoral.

Hii ina maana kama tutapanga kikosi kitakochaanza nadhani kitakuwa hivi: Navas; Carvajal, Varane, Ramos, Marcelo; Modric, Casemiro, Kroos; Bale, Benzema, Isco.
Kwa kuangalia kikosi hicho utaona kuwa endapo mabadiliko yatafanyika upande wa washambuliaji nje kuna Mayoral na Vazquez.
Tuangalie upande wa Barcelona:
Wachezaji ambao wapo na timu nchini Marekani ni:
Makipa: Cillessen, Ortola, Jokin
Mabeki: Pique, Alba, Digne, Umtiti, Vidal, Marlon, Douglas, Vermaelen, Semedo
Viungo: Busquets, Mascherano, Iniesta, Rakitic, Arda, D. Suarez, Roberto, Samper, Alena
Washambuliaji: Messi, Neymar, L. Suarez, Alcacer, Munir.
Kikosi ambacho tunafikiri kitaanza ni kama ifuatavyo: Cillessen; Semedo, Pique, Umtiti, Alba; Rakitic, Busquets, Iniesta; Messi, L. Suarez, Neymar.
Kwa kuangalia Barcelona utabaini asilimia kubwa wachezaji wao wapo na timu, hii ina mainisha kuwa Barcelona wanaweza kuwa faida kubwa ya kushinda mchezo huo ila Real Madrid na wao watataka kuonyesha kuwa bila Ronaldo wanaweza kuifunga Barcelona.

Mechi itakuwa 50% 50% japo mashindano haya hayana sare ni lazima mshindi apatikane.
Kwenye michuano hiyo Real Madrid ndio wanaburuza mkia baada ya kuambulia pointi 1 katika michezo 2 huku Barcelona wao wakiwa wanaongoza kituo hicho baada ya kushinda michezo yao yote miwili na kufikisha pointi 6.
Huku Neymar akiwa ndio anaongoza kwa kupachika magoli akiwa na goli 3
Siku ya mchezo: 29/07/2017
Uwanja: Hard Rock Stadium, Miami Gardens, Florida
Nchi: Marekani

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "ELCLASSICO KUPIGWA BILA RONALDO NCHINI MAREKANI, UCHAMBUZI NA UTABIRI"

Back To Top