Millionaire  Ads

Godfrey Nyange Kaburu na Evans Aveva Rumande mpaka july 13 2017



Rais wa Simba na Makamo wake wamerudishwa rumande hadi july 13, watuhumiwa hao wawili wanatuhumiwa kwa makosa matano ikiwemo kutakatisha fedha na kughushi nyaraka.
Makosa matano yanayowakabili ni kama ifuatavyo:
1. KUTAKATISHA FEDHA
Aveva alijipatia fedha kutoka Barclays bank tawi la Mikocheni.
2. KUGHUSHI
Aveva alighushi nyaraka ili kujilipa deni ambalo inadaiwa aliikopesha Simba USD 300,000.
3. KUTAKATISHA FEDHA KABURU
Kaburu alimsaidia Aveva kupata pesa USD 300,000 kutoka Barclays Bank tawi la Mikocheni.
4. KUTAKATISHA FEDHA
Tarehe tofauti Aveva na Kaburu walikula njama za kutakatisha fedha UDS 300000.
5. NYARAKA ZA UONGO
Walitumia nyaraka za uongo ili kulipa deni kutoka benki ya CRDB.
Kwa mujibu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kosa la utakatishaji fedha halina Dhamana hivyo watuhumiwa wamerudishwa Rumande hadi july 13 kupisha upelelezi kukamilika.





Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk " Godfrey Nyange Kaburu na Evans Aveva Rumande mpaka july 13 2017"

Back To Top