Millionaire  Ads

Bocco atua Afrika kusini, kurithi mikoba ya Mbaraka Yusuf


Mshambuliaji  mpya wa Simba, John Bocco ameongezwa katika kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania,Taifa Stars.
Bocco amejumuishwa katika kikosi hicho kufuatia kuumia kwa mshambuliaji Mbaraka Yusuph ambaye amekosa mechi mbili zilizopita za Taifa Stars dhidi ya Mauritius na Afrika Kusini. Tayari Bocco ameshajiunga na kambi ya Taifa Stars nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa mratibu wa taifa stars Ahmed Mgoi amesema wapo katika taratibu za kumsajili Bocco ili aweze kutumika katika michezo ijayo.
Mbarak yusuf jana alipelekwa Pritoria hospitali baada ya kupata tatizo la kiafya.
Kesho Taifa Stars inacheza mchezo mgumu dhidi ya timu ngumu ya Zambia katika hatua ya nusu Fainali.



Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Bocco atua Afrika kusini, kurithi mikoba ya Mbaraka Yusuf"

Back To Top