Millionaire  Ads

Arsenal waendeleza ubabe kwa vibonde wao Leicester City epl, wainyuka 4 - 3



Ligi kuu ya England maarufu kama EPL imeanza rasmi jana baada ya mabingwa wa FA na mabingwa wa ngao ya jamii timu ya Arsenal kuendeleza ubabe dhidi ya vibonde wao kwenye ligi timu ya Leicester City kwa kuidungua goli 4 – 3.

Alikuwa ni Alexandre Lacazette dakika ya 2 aliwaamsha wapenzi na mashabiki wa Arsenal baada ya kuukwamisha mpira wavuni kufuatia kazi nzuri ya Mohamed Elneny.
Shinji Okazaki alichomoa goli hilo dakika ya baada ya Harry Maguire kufanya kazi ya zaa dakika ya 5.
Dakika ya 29 Jamie Vardy aliongeza goli la pili  
Danny Welbeck alifunga la pili mnano dakika 3 za nyongeza za kipindi cha kwanza (45+3) akimalizia kazi kwa mchezaji anaekuja kwa kasi Saed Kolasinac.
Mpaka mapumziko Arsenal 2 – 2 Leicester.
Kipindi cha pili Jamie Vardy alifunga goli la tatu na la pili kwake dakika ya 56 mtengenezaji wa goli hilo alikuwa ni Riyad Mahrez.
Magoli mawili ya Arsenal yalifungwa na Aaron Ramsey na Olivier Giround

Mpaka mwisho wa mchezo Arsenal 4 – 3 Leicester.
Hivyo Arsenal wamendeza historia ya vipigo pindi wanapokutana na Leicester kwani historia inaonyesha kuwa tangu 31/8/2014 arsenal ametoka sare michezo miwili tu na kushinda michezo yote iliyobaki ya EPL.
Mechi yenye magoli mengi ni 5 -2 na  4 -3 idadi ikiwa magoli 7.
Takwimu kwa kifupi tangu 2014
31/8/2014 >>>>>Leicester 1 – 1 Arsenal
10/2/2015>>>>>Arsenal 2 - 1 Leicester
26/9/2015>>>> Leicester 2 – 5 Arsenal
14/2/2016>>>>>Arsenal 2 – Leicester
20/8/2016>>>> Leicester 0 – 0 Arsenal
26/4/2017>>>>Arsenal 1 – 0 Leicester
11/8/2017>>>>Arsenal 4 – 3 Leicester.

Kwa takwimu zilivyo hapo juu utakubaliana na mimi kuwa Leicester ni kibonde wa Arsenal kwenye EPL.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Arsenal waendeleza ubabe kwa vibonde wao Leicester City epl, wainyuka 4 - 3"

Back To Top