Millionaire  Ads

WANARIADHA WA TANZANIA KAZI IMEISHA JANA USIKU SASA KUREJEA TANZANIA


Wanariadha 8 walioiwakilisha Tanzania kwenye mashindano ya Dunia nchini uingereza katika jiji la London wanrejea nchini wakiwa na medali moja tu ya Shaba ambayo mtanzania Alphonce Simbu ndie aliyeitwaa siku chache zilizopita.
Jana watanzania wawili ilikuwa wakimbie kwenye hatua ya fainali lakini alikimbia mwanariadha mmoja na kuambulia nafasi ya 13 hivyo kukosa nafasi ya kutinga fainali zitakazo fanyika siku ya jumamosi august 12.
Mtanzania aliekimbia jana ni Emmanuel Ginik
Giniki baada ya mashindano alisema “kiukweli mashindano yalikuwa ni magumu na niliweza kujitahidi kwa kadri nilivyoweza lakini kwa bahati mbaya kabsa kilichonitokea nilikuja kukanyangwa mguu ilipobbaki mita 800 sasa nilishindwa kushindana kwa ile hali ya kupiga kiki ndio ikawa sio bahati yangu tena”
Katibu alimpongeza Giniki kwa kumaliza mbio
“ujuzi ndio uliomuangusha Ginik na kujikuta kaingia kwenye boksi na kushindwa kutoka na ndio pale akakanyangwa, lakini nampongeza sana kwa kumalizwa mbio”alisema Gidabudai
“nimepata kuona maono ya Filibert Bay akimtabiria Ginik kuwa atatumia dakika 13 na kuvunja rekodi ya taifa”aliendelea kusema.
Kuhusu mwanariadha Gabriel Gerald Gea ambae alitakiwa kukimbia mbio hizo lakini hakuonekana  gidabudai alisema “Gea alikuwa akimbie na aliwekwa kwenye hit no two lakini hakuanza mbio  kwa sababu ya msituko wa goti,makocha wawili na mimi tulikaa kulipeleka tatizo lake kwa madaktari ambao wapo na jana waliamua kuwa Gea hatoweza kukimbia”  

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "WANARIADHA WA TANZANIA KAZI IMEISHA JANA USIKU SASA KUREJEA TANZANIA"

Back To Top