Millionaire  Ads

Msuva atoa neno baada ya kukutwa na Hatia ya kumsukuma


Kamati ya nidhamu ya TFF jana August 31, 2017 ilitangaza kumuandikia barua ya onyo kali winga wa Taifa Stars na klabu ya Difaa El Jadid ya Morocco Simon Msuva baada ya kumkuta na hatia ya kumsukuma mwamuzi kwenye mechi ya mwisho ya ligi kuu Tanzania bara msimu uliopita kati ya Mbao FC dhidi ya Yanga kwenye uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Sakata hilo liliwahusu wachezaji watatu ambao awali walikuwa wanaitumikia timu ya Yanga ambao ni Obrey Chirwa na Deus Kaseke Pamoja na Simon Msuva, lakini kwa sasa aliyebaki Yanga ni Chirwa peke yake wakati Kaseke akisajiliwa na Singida Utd na Msuva akijiunga na Difaa El Jadid ya Morocco.
Msuva baada ya kukutwa na hatia aliomba radhi sana na kuwaasa wachezaji wengine wayaheshimu maamuzi ya refa awapo uwanjani.
“Maamuzi waliyotoa nayapokea kwa sababu hata kwa wachezaji wengine itawafundisha kwamba, maamuzi anayotoa refa ndio hayohayo ameamua kutoa. Naomba radhi kwa kilichotokea kwa sababu hakikutokea kwa pekeangu, tulikuwa wachezaji watatu mimi, Chirwa na Kaseke, mimi naomba radhi na wao najua wataomba radhi kwa muda wao,” alisema Simon Msuva.



Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Msuva atoa neno baada ya kukutwa na Hatia ya kumsukuma "

Back To Top