Millionaire  Ads

TOP SCORES LIGI KUU UINGEREZA, MORATA, LUKAKU na AGUERO KAZI IPO MWAKA HUU




Washambuliaji wa ligi kuu nchini Uingereza wanaonekana hawataki mzaha msimu, na hili halipingiki miongoni mwa wadau wengi wa soka ulimwenguni.
Chelsea wamemsajili Alvaro Morata kama mrithi wa Diego Costa ambae kulitokea sintofahamu kati yake na kocha wa timu hiyo Conte hivyo kulazimika kumpiga bei kwenda Atletico Madrid.
Ujio wa Morata watu waliubeza lakini kiwango alichokionyesha mchezaji huyo tunaweza kusema dunia haiwezi kuhamaki mwisho wa msimu akiwa mfungaji bora.
Kwanza amevunja rekodi ya Diego Costa ya kufunga magoli matatu katika mchezo mmoja hat trick jana dhidi ya Stock City rekodi ambayo iliwekwa na Costa tangu 2014 katika mchezo kati ya Chelsea na Swansea City.
Mpaka sasa ana goli 6 katika michezo sita ya ligi kuu nchini Uingereza.
Lukaku anaendelea kuwathibitishia walimwengu kuwa thamani ya euro milioni 75 ilikuwa sahihi kwake kama dau la uhamisho toka Everton kwenda Man UTD.
Lukaku mapaka sasa ameshafunga magoli 6 katika michezo sita ya ligi kuu nchini Uingereza.
Kama kawaida yake tayari ameshafunga goli 6 na nadhani msimu huu kutokana na jinsi washambuliaji wa timu pinzani walivyo lazima afunge zaidi ili kuiaminisha Dunia kuwa yeye bado yupo na kazi yake ni moja tu ya kucheka na Nyavu

Baada ya vuta ni kuvute ya kutakiwa na mzee Wenger kama mbadilishano na Sanchez Raheem anaithibitishia dunia kuwa haikuwa sahihi kwake kutolewa yeye pamoja na pesa kwa ajili ya dili la kumnasa Sanchez mpaka sasa amefunga goli 5.

Miongoni mwa washambuliaji asili kwa sasa duniani ni pamoja na Vardy, Vardy mpaka sasa amefunga magoli 5 na bado anaweza kuendelea kufunga nahii anauaminisha umma wa wapenda soka kuwa yeye ni miongoni mwa washambuliaji bora kabisa kwa sasa
Huyu ndie mfungaji bora wa msimu uliopita na kuna uwezekano akatetea kiatu chake endapo atauendeleza moto alioanza nao mpaka sasa ana goli 4.
 takwimu ya wafungaji kwa kifupi ipo hivi:


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "TOP SCORES LIGI KUU UINGEREZA, MORATA, LUKAKU na AGUERO KAZI IPO MWAKA HUU"

Back To Top