Millionaire  Ads

Mkubwa mkubwa tu hatimae Ureno ya Ronaldo na Argentina ya Messi ndani ya kombe la Dunia mwakani nchini Urusi



Mkubwa mkubwa tu hatimae Ureno ya Ronaldo na Argentina ya Messi ndani ya kombe la Dunia mwakani
Hatimae Lionel Messi ameweza kuibeba timu yake ya taifa na kuipeleka fainali za mwakani za kombe la Dunia baada ya jana kuifungia magoli muhimu matatu.
Messi alifunga magoli hayo dakika za 11,18 na 62 na kuifanya Argentina kuifunga Ecuador 3 – 1.

Kwa Matokeo hayo ya ushindi wa jana yanaifanya Argentina kushika nafasi ya 3 kwa kujikusanyia  jumla ya pointi 28 nyuma ya vinara Brazil wenye pointi 41 na Uruguay wenye point 31
Kwa upande mwingine Ureno ya Ronaldo imefanikiwa kuongoza kundi B baada ya ushindi wa goli 2 – 0 dhidi ya waliokuwa vinara wa kundi hilo Switzerland.
Kwa mantiki hiyo Ureno wamefungana pointi na timu ya Switzerland kila timu ina pointi 27 isipokuwa Ureno wao wanamtaji mkubwa wa magoli ya kufunga na kufungwa.
Ureno wamefunga magoli 32 na kufungwa 4 huku Switzerland ikiwa imefunga magoli 23 na kufungwa 7.
Ukiangalia takwimu hapo Ureno anautofauti wa magoli 28 wakati hasimu wake huyo ana utofauti wa magoli 16.
Magoli ya Ureno yalifungwa na Johan Djourou alijifungwa kwenye dakika ya 41 na goli la pili lilifungwa na Andre Silva dakika ya 57


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Mkubwa mkubwa tu hatimae Ureno ya Ronaldo na Argentina ya Messi ndani ya kombe la Dunia mwakani nchini Urusi"

Back To Top