Millionaire  Ads

NDANDA WAAHIDI USHINDI MNONO SIKU YA KESHO DHIDI YA MATAJIRI SINGIDA UNITED



Timu ya ndanda ya mkoani mtwara leo mchana imewatoa hofu wadau na mashabiki wa timu hiyo popote pale walipo kuwa lazima Singida Utd kesho waziachie pointi tatu ndani ya dimba la Nangwanda mjini Mtwara.
Akizungumza na waandishi wa habari Saidi Limbega ambae ni mweka hazina wa Ndanda alisema “sisi kama timu tumejiandaa vizuri na kikosi chetu kipo imara kwa mapambano ili kuweza kupata pointi tatu, tunahakika ndanda ni wazuri zaidi ya Singida UTD,” “niwaombe wapenzi na mashabiki waje watusapoti kwa sababu washangiliaji ni mchezaji wa 12 ” alisisitiza Limbega.

Limbega pia amesema baada ya mchezo huo timu itapata mapumziko kwa siku mbili kabla ya maandalizi ya safari ya Bukoba kwa mchezo ujao dhidi ya Kagera 
Ndanda wapo nafasi ya 8 baada ya kucheza michezo 6 na kujikusanyia pointi 8.
Singida UTD wao wapo nafasi ya 5 wakiwa na pointi 11 baada ya michezo 6

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "NDANDA WAAHIDI USHINDI MNONO SIKU YA KESHO DHIDI YA MATAJIRI SINGIDA UNITED"

Back To Top