Millionaire  Ads

YANGA IMEANZA SAFARI YA KUSAKA POINT TATU KAMBARAGE


Mabingwa watetezi wa  ligi kuu Tanzania Bara timu ya Yanga mchana huu wameelekea mkoani Shinyanga wakitokea Tabora ambapo waliweka kambi ya muda kwa ajili ya maandalizi ya mchezo dhidi ya Stand United.
Yanga wanaenda Kambarage wakiwa na kumbukumbu ya kipigo cha golui 1 kwa 0 msimu uliopita katika uwanja huo.
Lilikuwa ni goli la Pastory Atanas ambae kwa sasa anaitumikia timu ya Singida United ndio lililoifanya Yanga msimu uliopita kuuona uwanja wa kambarage kuwa na mchungu
Hivyo mchezo wa Jumapili utakuwa mgumu kwa timu zote mbili kwani Yanga wanataka kulipiza kisasi cha msimu uliopita na kujiweka vizuri kwenye msimamo wa Ligi Kuu.

Stand United wanataka kupata ushindi ili kujinasua mkiani kwani mpaka saa wana pointi nne huku wakiwa katika nafasi ya 15.

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "YANGA IMEANZA SAFARI YA KUSAKA POINT TATU KAMBARAGE"

Back To Top