Millionaire  Ads

NDANDA YAWAKANA WAZAMINI NA KUONDOA MABANGO YAO UWANJANI



Timu ya Ndanda ya mkoani mtwara imewakana wazamini wake wawili kampuni ya kiboko na Maxcom Lmtd.
Hayo yameibuka baada ya wadau kuanza kuushutumu uongozi kuwa timu inalia ukata wakati timu ina wazamini wane.
George Njooka ambae ni katibu mkuu wa timu ya Ndanda amesema wadhamini wanaowatambua ni Azam Tv na Vodacom na ndio wanaotoa fedha ndani ya timu hiyo.
Aliwazungumzia kiboko “Kiboko yupo anaitwa mdhamini kwa maana ya kwamba kile kipindi ambacho timu ya Ndanda kuna wenzetu walitoka Dar es salaam wakawa wanataka kuungana na sisi kuendesha timu na sisi tuliwakaribisha kuendesha timu wao kabla mamboyote hayajakaa vizuri wakatafta wadhamini wakaenda kusaini mkataba na kiboko lakini utaratibu wetu timu ya Ndanda inaongozwa na bodi ya wakurugenzi ” alisema Njooka.

Nae mwekahazina wa Ndanda amekiri kupokea fedha toka kwa Azam Tv na Vodacom tu na hajapokea fedha nyingine yoyote.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "NDANDA YAWAKANA WAZAMINI NA KUONDOA MABANGO YAO UWANJANI"

Back To Top