Millionaire  Ads

RONALDO KUAMUA NAFASI YAO YA KUFUZU KOMBE LA DUNIA LEO MBELE YA VINARA SWITZERLAND



Timu ya taifa Ureno leo mida ya saa nne kasorobo itakuwa na kibarua kigumu cha kupata tiketi ya moja kwa moja kufuzu kombe la Dunia nchini urusi.
Ureno endapo watapata ushindi wowote leo watakuwa wanawapiku vinara wa kundi hilo uongozi wa kundi kwa uwiano mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa.
Mpaka sasa Switzerland wana pointi 27 wakati Ureno wana pointi 24.
Mpaka sasa Switzerland wamefunga magoli  23 na wamefungwa magoli 5 wakati Ureno imefunga magoli 30 na kufungwa magoli 4.
Hivyo ukiangalia takwimu hizo zinambeba Ureno endapo atashinda mchezo huo.
Lakini Switzerland sio wakubeza kwani katika mchezo wa Sep 6, 2016 walipata ushindi wa goli 2 – 0 mbele ya Ureno kwa magoli ya Breel Embolo dakika 24 na Admir Mehmedi dakika 30 huku Granit Xhaka akipewa kadi nyekundu dakika ya 90 na huo ulikuwa ni mchezo wa raundi ya kwanza katika kundi.
Katika mchezo huo Ronaldo hakucheza na huenda uwepo wake kwa siku ya leo ukaongeza kitu na Ureno kupata nafasi ya moja kwa moja mbele ya mashabiki wake.


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk " RONALDO KUAMUA NAFASI YAO YA KUFUZU KOMBE LA DUNIA LEO MBELE YA VINARA SWITZERLAND"

Back To Top