Millionaire  Ads

Ujerumani, Ubelgiji, Uingereza zimekata tiketi ya kombe la Dunia Ureno bado mambo magumu




Mpaka  sasa timu zote barani Ulaya zimebakisha mchezo mmoja mmoja ili kumaliza  mchujo wa kupata timu ambazo zitafuzu moja kwa moja kwa kombe la Dunia nchini Urusi mwakani.
Kuna baadhi ya makundi tayari mambo yameshaeleweka lakini kuna makundi mengine ambayo bado ngoma ni mbichi mpaka mchezo wa mwisho ndio hatima ya nani anaenda Urusi na nani atacheza mchezo wa mtoano yaani Play OFF.
Katika makala hii tutapitia makundi yote kuanzia kundi A – I

Tukianza 
 kundi A.

Bado haijajulikana nani atapata tiketi ya moja kwa moja angalia Msimamo kwenye kundi hapo juu.
Ufaransa anaongoza kundi A kwa pointi 1 mbele ya Sweeden hii inategemea na mchezo wa mwisho ambapo kwa ufaransa ni ushindi tu ndio utawahakikishia tiketi bila kujali Matokeo ya timu nyingine.
Michezo ya mwisho kwa kundi hili itapigwa mapema Tarehe na muda kama unavyoonekana hapo chini
Kundi B.

Kundi hili tayari timu mbili za juu zishajitenga ikimainisha kinara wa ligi ambae anahitaji pointi moja tu ili aweze kwenda Urusi mwakani wakati Ureno ya Ronaldo bado inanyatia nyatia huku ikiiombea dua mbaya Switzerland ifungwe kwa kuwa Ureno ina mtaji mzuri wa magoli ya kufunga na kufungwa.
Mechi za mwisho zitakuwa kama ifuatavyo hapo chini:

kundi C:

Timu ya Ujerumani tayari imefuzu kabla ya kucheza mchezo wa mwisho wakati huohuo Ireland kaskazini nayo imefuzu kwa hatua ya mtoano Play Off.
Michezo ya mwisho itakuwa kama hivi:


 kundi D:

Timu tatu za juu zote zinanafasi ya kupata tiketi ya kwenda urusi mojamoja inategemea na jinsi zitakavyo zichanga karata zake siku ya mwisho.
Hili ndio kundi pekee ambalo inawezekana kinara akashindwa kufuzu na akakosa hata Play Off
Michezo ya mwisho itakuwa hivi:

kundi E:

Kundi hili timu tatu za juu zina nafasi sawa ya kucheza play Off lakini Montenegro yenyewe imeshajitoa katika mbio za kuwania nafasi ya moja kwa moja na kuziachia timu mbili za juu.
Japo Poland wana asilimia kubwa ya kufuzu licha ya amsha amsha ya Denmark.
Ila Kutokana na mchezo wa mwisho endapo Montenegro atashinda na Denmark akashinda kuna uwezekano mkubwa Poland akaishia nafasi ya pili.
Michezo ya mwisho itakuwa kama hivi:
kundi F:

Kundi hili England tayari washafuzu imebakia nafasi ya pili ambayo inagombewa na timu tatu kama inavyoonekana hapo juu.
Msimamo ulivyo Scotland lazima ashinde ili ajihakikishie nafasi kinyume na hapo mambo yanaweza kugeuka.
Endapo atasuluhu halafu Slovakia akashinda kwa idadi yoyote ya mabao basi safari ya Scotland itaishia hapo.
Michezo ya mwisho itapigwa leo majira ya saa moja usiku na mpaka saa tatu tutajua ni taifa gani limefuzu kwa hatua ya mtoano

kundi G:

Kundi hili tayari lishafamika nani ni nani tayari kama linavyoonekana kwa nafasi mbili za juu.
Watakamilisha Ratiba tu kwenye michezo ya mwisho:
kundi H:
Kundi hili nafasi inayogombaniwa ni nafasi ya pili baada ya Ubeligiji kutwaa nafasi ya kwanza.
Timu iliyonafasi ya tatu na nafasi ya pili moja wapo inaweza kutwaa nafasi ya pili.
Mechi za mwisho zitakuwa hivi:

kundi I
Hili nalo ni kundi la kifo na litaamuliwa na michezo ya mwisho kila timu kuanzia nafasi ya tatu zina nafasi ya tiketi ya moja kwa moja na kila timu ina nafasi ya kucheza play off ila na Uturuki nae endapo atashinda goli 9 kuna uwezekano nae akatinga nafasi ya pili.

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Ujerumani, Ubelgiji, Uingereza zimekata tiketi ya kombe la Dunia Ureno bado mambo magumu "

Back To Top