Millionaire  Ads

Ranieri apigiwa chapuo ukocha Palermo


Palermo wapo mbioni kumpa ulaji wa kuinoa timu hiyo Claudio Ranieri.

Rais wa kilabu ya Palermo Paul Baccaglini anataka kumpa nafasi ya ukocha, aliyewahi kuwa kocha kwa mafanikio makubwa na timu ya Leicester muitaliano Claudio Ranieri.

Palemo ambayo inapigana kumbo kuepuka kushuka daraja msimu huu, inataka kumchukua Ranieri ili aweze kuinusu timu hiyo na janga la kushuka daraja.

Rais huyo mpya anadhani Ranieri ndio chaguo sahihi kwani alishawahi kuichezea timu hiyo hvyo anajuwa mazingira ya Stadio Renzo Barbera.

Palermo ipo katika nafasi ya 18 kati ya timu 20, ina pointi 15 katika michezo 29, katika michezo yote hiyo Palemo imeshinda michezo matatu tu na kutoka sare michezo 6.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme
0 Comment untuk "Ranieri apigiwa chapuo ukocha Palermo"

Back To Top