Millionaire  Ads

Refa wa kombe la duniani kuchezesha mechi ya Yanga na Azam jumamosi april 1


Refa pekee kutoka Tanzania ambae ameteuliwa na shirikisho la mpira wa miguu duniani kuchezesha fainali za kombe la dunia kwa wanawake mwaka 2019 huko Ufaransa ndie muamuzi mchezo kati ya Azam na Yanga.
Ikumbukwe kuwa zinapokutana mara nyingi timu hizi mbili mchezo huwa mgumu na wenye hisia tofauti kwa waamuzi.
Tff wamempa jukumu mwanadada Jonesia Rukyaa jukumu la kushika firimbi kuamua mchezo huo ambao ni muhimu kwa kila timu.
 Ikumbukwe kuwa mwanadada huyo amewahi kuchezesha michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wanawake iliyofanyika Cameroon mwaka jana na kuwa mwamuzi wa kwanza wa kike nchini kuchezesha michuano hiyo mikubwa barani Afrika
Rukyaa amewahi kuchezesha mchezo kati ya Yanga na Simba mtani jembeambapo simba waliibuka washindi kwa 3 - ,  pia mchezo Yanga na Simba mchezo wa raundi ya pili ligi kuu Tanzania Bara ambapo Yanga walishinda 2 – 0.

Katika michezo hiyo hakujakuwa na malalamiko hivyo Tff huenda wakamchagua Yeye Kutokana na uzoefu alionao kwa michezo yenye msisimko kwa wadau wengi wa soka.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+
0 Comment untuk "Refa wa kombe la duniani kuchezesha mechi ya Yanga na Azam jumamosi april 1"

Back To Top