![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgUN35nTlyQX442ylprzo7mfwLsdbgntbToN91PqqPiR-f2uMGvWcqM4RZpt9_y0KjgvAIiDoVs5O839t83eaNBKta1xmlTyqSXI3uGa4ssVHU5JADV_En6Zw7u89H7uL5fAZiMVd8XNB4/s640/tp.jpg)
Ratiba ya kombe la shirikisho Azam
confederation Cup kati ya Azam na Ndanda toka mkoani mtwara katika hatua ya
robo fainali sasa kupigwa April 5 Chamanzi Complex saa moja usiku.
Awali mchezo huo ulipangwa kufanyika
kati ya Machi 18 na 19 mwaka huu, lakini ulisogezwa mbele kutokana na Azam FC
kuwa kwenye majukumu ya mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi
ya Mbabane Swallows ya Swaziland ambapo Azam alitolewa kwa jumla ya 3 -1.
Mbali na mechi hiyo ya Azam FC,
mtanange mwingine uliobakia utafanyika Aprili 22 mwaka huu kati ya mabingwa
watetezi Yanga na Tanzania Prisons, utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Mshindi wa michuano hiyo iliyorejea
msimu uliopita, anatarajia kujishindia kombe pamoja na kitita cha Sh. milioni
50 na kuiwakilisha Tanzania Bara kwenye Kombe la Shirikisho Afrika mwakani.
Millionaire Ads
0 Comment untuk "Azam vs Ndanda April 5, Yanga vs Prisons April 22 robo fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup)"