Millionaire  Ads

Stars yafanya kweli South Afrika, yaitungua Malawi 2 - 0



Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars leo imeanza vyema mashindano ya COSAFA baada ya kuitandika bila huruma timu ya Malawi kwa jumla ya goli 2 – 0.
Iliwachukua Stars dakika 13 baada ya mchezo kuanza kuandika goli la kwanza likiwekwa wavuni na kiungo mshambuliaji Shiza Kichuya.
Dakika tano badae yaani dakika ya 18 kichuya Tena aliuwahi mpira ambao ulikuwa unaelekea kwa mtu na kuukokota na badae kupiga shuti la ufundi kwa kutumia mguu wake wa kushoto na kumshinda mlinda mlango wa Malawi akiruka bila mafanikio.
Mpaka mapumziko ilikuwa 2 – 0.
Kipindi cha pili Malawi walionekana kucheza zaidi kupitia upande wa kushoto lakini Gadiel Michael na Abdi Banda waliweza kuwazua washambuliaji wa Malawi.
Maajabu ya leo ni mabadiliko aliyofanya kocha wa Taifa Stars ya kuwatoa viungo washambuaji wote wawili na kuingiza mabeki.
Alimtoa Kichuya akamuingiza Hassan Kessy, akamtoa Msuva akamuingiza Chona.
Pia alimtoa mshambuliaji Elias Maguri na kumuingiza ‘Samatta mpya’ MbarakYussuf ambae aliwasumbua atakavyo mabeki wa Malawi.

Hadi mwisho wa mchezo Tanzania 2 – 0 Malawi.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Stars yafanya kweli South Afrika, yaitungua Malawi 2 - 0"

Back To Top