Millionaire  Ads

Kamati yamtoa Manara kifungoni



Kamati ya nidhamu ya shirikisho la soka nchini Tanzania TFF chini ya mwenyekiti wake Tarimba Abbas imeamuachia huru Manara na baadhi ya wadau wengine wa soka waliokuwa kifungoni kwa vipindi tofauti.
Sababu za kuachiwa huru kwao ni Kutokana na baadhi yao akiwemo manara kuiandikia kamati hiyo kuipitia upya hukumu yao na kuomba wapunguziwe adhabu hizo walizopewa.
Kamati imewaacha rasmi huru wafuatao:
1.    Haji Manara msemaji wa timu ya Simba SC
2.    Ayubu Myaulingo ambeye ni mwenyekiti wa Chama cha Soka mkoa wa  Rukwa.
3.    Blassy kiondo ambaye ni kaimu katibu mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Rukwa
4.    James Makwinya Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi Rukwa

Tarimba amesema "Wale ambao hawakuwasilisha kutaka kupitiwa upya kwa hukumu zao, tumewaambia TFF nao walifanyie kazi hilo. Kama watataka kuona inafanyika review basi haki itendeke"
Baada ya kupata msamaha huo Manara aliahidi yafuatayo:
“Nawaahidi kuendelea kufanya kazi zangu kwa weledi, nidhamu na kwa kuzingatia miiko ya mchezo huu, unaobeba dhamana za maisha ya watu walio wengi, sambamba na kuendelea kuitetea na kuilinda klabu yangu kwa nguvu zote,”.
Hayo ni maneno ya Manara


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Kamati yamtoa Manara kifungoni"

Back To Top