Millionaire  Ads

RIPOTI YA MADAKTARI: NGOMA RUKSA KUICHEZEA YANGA MSIMU HUU, DIDA NAE AANZA MAZOEZI NA YANGA


Ripoti toka kwa madaktari wanaomtibu mshambuliaji wa timu ya Yanga Donald Dombo Ngoma wamemruhusu mchezaji huyo kuanza mazoezi baada ya vipimo vya mwisho kuonyesha kuwa yupo ‘FIT’.
Ngoma atajiunga na wenzake ndani ya wiki hii baada ya kurejea kutoka Afrika Kusini alipokwenda kufanyiwa vipimo kilisema Chanzo cha habari hiyo.
Ngoma ambae alikuwa gumzo baada ya kuhusishwa kujiunga na Simba lakini alirejea na kusaini mkataba wa miaka miwili na Yanga.
Ujio wa Ngoma ni furaha tosha kwa mashabiki na benchi la ufundi ambapo sasa litakuwa na wigo wa kuamua nani aanze kikosi cha kwanza baina ya wachezaji Ngoma, Chirwa, Tambwe na Ajib.
Wakati huohuo kipa namba moja ndani ya Yanga Deo Munish ameanza mazoezi na timu ya Yanga kwa ajili ya maandalizi ya ngao ya jamii, msimu mpya wa ligi, kombe la shirikisho la Azam na kilab bingwa Afrika.




Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "RIPOTI YA MADAKTARI: NGOMA RUKSA KUICHEZEA YANGA MSIMU HUU, DIDA NAE AANZA MAZOEZI NA YANGA"

Back To Top