Millionaire  Ads

NDANDA KUANZA MAZOEZI RASMI KESHO TAYARI KWA MSIMU UJAO



Msemaji wa timu ya Ndanda ya mtwara wana kuchele Indrisa Bandari ameiambia jamii fm Radio ya mkoani mtwara kuwa timu yao kesho jumatatu inaanza rasmi mazoezi ya kujiandaa na ligi kuu Tanzania Bara."tutafanya mazoezi mara mbili kwa siku, asubuhi na jioni," alisema Bandari
Kuhusu suala la timu kutokuwa na kocha Bandari alisema kuanzia sasa muda wowote watamtangaza kocha wao, wapo kwenye mazungumzo ya kukamilisha mkataba.
Alipoulizwa kuhusu fukuzafukuza ya makocha ndani ya timu hiyo bandari alisema "ndanda haifukuzi mwalimu tunaangalia ‘commitments’ ya mkataba ipoje, tunaangalia mkataba wake upoje akishindwa kufikia matarajio ya mkataba, mwalimu anaondoka".
Kuhusu suala la usajili Bandari aliwataja baadhi ya wachezaji ambao mpaka sasa wameshasajiliwa na timu hiyo kuwa ni Ibrahim Job, Jabir Azizi, na kuahidi kuwa wapo vijana wengine watano ambao anategemea kuwatangaza kesho.


Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "NDANDA KUANZA MAZOEZI RASMI KESHO TAYARI KWA MSIMU UJAO"

Back To Top