Millionaire  Ads

Samatta aliamsha dude Belgium - First Division A, atupia na kutengeneza moja




Mtanzania Mbwana Samatta jana usiku alifanya kile kinachotabiriwa na wengi huenda akawa mfungaji bora wa Belgium baada ya jana kuanza vyema.
Genk na Waasland-Beveren walitoka sare ya 3- 3 lakini kitu kizuri kwa watanzania ni nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania kufanya yake.
Waasland-Beveren ndio wa kwanza kujipatia magoli mawili, dakika ya 45 Oliver Myny alifunga goli la kwanza, mnamo dakika ya 47, Zinho Gano alipachika goli la pili na kufanya wageni hao waongoze kwa goli hizo mbili.
Genk walisubiri mpaka dakika ya 70 ndio wakafungua ukurasa wa magoli kupitia kwa Naranjo, 80’ Samatta akachoa na ubao ukasomeka 2 – 2.
Dakika ya 82 Genk kupitia kwa Leandro Trossard walipata goli la 3.


Wakiamini kuwa mpira umeisha ghafla dakika ya 90 Waasland-Beveren kupitia kwa Zinho Gano walisawazisha na mchezo kuhitimishwa kwa sare ya  3 – 3.

matokeo mengine ni:

Lokeren 0 - 4 Club Brugge
Eupen 0 - 5 Zulte-Waregem

Sporting Charleroi 1 - 0 Kortrijk
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Samatta aliamsha dude Belgium - First Division A, atupia na kutengeneza moja"

Back To Top