Millionaire  Ads

Shirikisho la Mpira barani Afrika CAF linafanya mkutano wa siku mbili nchini Morocco

Moja ya mada kuu zitakazojadiliwa ni uwezekano wa kubadili kalenda ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika ili isiingiliane na ratiba ya ligi za Ulaya. Kombe la Mataifa hufanyika mwezi Januari wakati ligi za Ulaya zimepamba moto, na wachezaji muhimu hulazimika kwenda kuchezea timu zao za taifa, pia watajadili kuhusu mashindano yaliyochini ya CAF ngazi ya vilabu nk.
Mkutano huo utaongozwa na Ahmad Ahmad ambae ndie rais wa sasa wa CAF aliyechukua mikoba ya Rais aliyedumu kwa miaka 29 ndani ya Shirikisho hiyo Issa Hayatou.

Wadau mbalimbali wapatao zaidi ya 400 wanategemewa kuhudhuria mkutano huo akiwemo kocha wa mabingwa wa ligi ya MabingwaUlaya Real Madrid  Zinedine Zidane. 

Hayo yanafanyika kabla ya mkutano mkuu wa CAF utakaofanyika july 20 na july 21 na kuwashirikisha washirika wake wote 56.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk " Shirikisho la Mpira barani Afrika CAF linafanya mkutano wa siku mbili nchini Morocco"

Back To Top