Millionaire  Ads

YA YANGA KUWAKUTA SIMBA



Timu ya simba SC inaweza kumuuza mchezaji wake tegemeo kwenye nchi za kiarabu Chanzo kimoja kimeeleza.
Shiza Kichuya huenda nae akafuata nyao za Saimon Msuva kutimkia nchi za kiarabu baada ya timu moja ambayo haijatajwa jina lake kuvutiwa na mchezaji huyo.
Timu hiyo ipo tayari kumfanyia vipimo vya afya pekee na kumjuisha katika kikosi chao bila majaribio endapo atafuzu vipimo.
Kwa Tanzania ni mwanzo mzuri kwani baada ya msimu ulioisha wa ligi kuu kumalizika wachezaji maarufu watatu wamepata timu nje ya nchi tena za ligi kuu.
Wachezaji hao ni Abdi Banda toka Simba aliyetua Baroka Fc Afrika kusini, Ramadhani Singano ‘Messi’ toka Azam na Saimon Msuva toka Yanga wawili hawa wapo Difaa Aljadida ya Morocco.

Huu ni mwanzo mzuri kwa soka letu hasa timu ya taifa.
ikumbukwe pia kiungo wa timu ya Simba Said Ndemla na yeye ametimkia Swedeen kufanya majaribio.

Mungu zibariki Safari za wachezaji wetu Amin.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "YA YANGA KUWAKUTA SIMBA"

Back To Top