Millionaire  Ads

MSUVA ACHAGULIWA KUTAMBULISHA JEZI ZA DIFAA HASSANI JADIDI


Mchezaji mpya wa Difaa Hassani Jadidi ya nchini Morocco, mtanzania Simon Msuva ni miongoni mwa wachezaji waliochaguliwa kutambulisha jezi za timu hiyo kwa msimu ujao.
Na baada ya utambulisho huo timu hiyo ilishuka uwanjani kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya ASO  Daraja la Kwanza.
Katika mchezo huo Msuva alifunga goli moja na kutengeneza goli la ushindi.
Matokeo yalikuwa  2-1 kwa difaa kushinda mchezo huo.

“Tumeshinda mabao 2-1, maana huku kila siku tunacheza mechi, kweli wenzetu wapo tofauti sana,”amesema Msuva na kuongeza; “Leo mimi nimefunga la kusawazisha na kutengeneza la ushindi,”.

“Ni mechi ngumu, timu za huku wachezaji wake wapo fiti sana na wana nguvu na kasi sana, kwa kweli huku wenzetu wapo tofauti sana,”alisema.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "MSUVA ACHAGULIWA KUTAMBULISHA JEZI ZA DIFAA HASSANI JADIDI"

Back To Top