Millionaire  Ads

Cristiano, Messi na Neymar wapitishwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa FIFA (The Best FIFA Men's)


Cristiano, Messi na Neymar wapitishwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa FIFA (The Best FIFA Men's)
Awali majina yalikuwa 24 lakini yamechujwa na kubakia majina 3.
Wanaofanya kazi hii ni jopo la makocha wa timu za taifa,makeptein wa timu za taifa, baadhi ya vyombo vya habari vilivyo chaguliwa na wadau wa soka.
Majina hayo 24 yalianza kuchujwa tangu  August 21 na September 7

Majina yaliyobahatika kubaki ni Cristiano, Messi na Neymar na utoaji wa tuzo hizo utafanyika October 23 huko London Uingereza.

Kuna uwezekano mkubwa kwa mchezaji bora Duniani raia wa Ureno Cristiano Ronaldo kutetea taji lake la FIFA Best Player of the year.
Uwezekano huo unatokana na mafanikio aliyoyapata kwa msimu ulioisha ukilinganisha na  wapinzani wake Messi na Neymar.
Ronaldo ambae kwa msimu ulipita aliisaidia timu yake ya taifa kutinga nusu fainali ya kombe la mabara, aliweza kuisaidia kilabu yake kutwaa ligi ya mabingwa Ulaya, Laliga Pamoja na Uefa Super Cup, huku Ronaldo akimpiku Messi kwenye ufungaji bora wa ligi ya mabingwa Ulaya.

Kwa upande wa Messi yeye msimu uliopita alitwaa tuzo ya mfungaji bora wa laliga na kuambulia kikombe kimoja tu cha Copa del Rey.

Neymar ambae ndie mchezaji ghali zaidi Duniani akisajiliwa toka Barcelona kwenda PSG anapewa nafasi ndogo ya kutwaa tuzo hiyo.
Angalia rekodi zao za ufungaji kuanzia  November 20,2016 mpaka July 2 2017

Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Cristiano, Messi na Neymar wapitishwa kuwania tuzo ya mchezaji bora wa FIFA (The Best FIFA Men's)"

Back To Top