Millionaire  Ads

Kuziona Simba na Yanga jumamosi Tshs.10000 uwanja wa Uhuru



Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania TFF limetangaza viingilio katika mchezo ujao wa watani wa jadi Simba na Yanga siku ya jumamosi October 28.
Viingilio vitakuwa kama ifuatavyo:
Mzunguko: tshs 10000
Jukwaa kuu: tshs 20000
Mchezo huo ambao utapigwa kwenye dimba la Uhuru jijini Dar es Salaam unasubiriwa kwa hamu na wadau wengi wa soka ndani na nje ya Tanzania.
Tambo zimezidi kuongezeka hasa ukiangalia Matokeo ya michezo ya mwisho ya timu hizo ambapo Simba waliitandika Njombe mji goli 4 – 0 huku Yanga nao wakiitandika Stand United ya Shinyanga kwa goli 4 – 0.
Tukurudi kwenye ‘performance’ ni kama timu zote ziko sawa kwa maana zote zimecheza michezo 7 na kushinda kushinda 4, kutoka sare 3 na zote zina pointi 15.
Simba yenyewe inaonekana kuwa na safu kali zaidi ya ushambuliaji kwa mujibu wa takwimu ambazo zipo katika michezo hiyo saba Simba imefunga magoli 19 wakati yanga ikiwa imefunga magoli 10 pekee.
Kwa upande wa ulinzi Yanga wao wapo vizuri zaidi ya Simba kwa kuruhusu magoli matatu tu katika michezo saba wakati Simba wao wameruhusu magoli 4.
Tutegemee mchezo ambao utakuwa na ushindani wa hali ya juu, ukiingalia Simba imeleta kocha msaidizi ambae wadau wanategemea atakuja na mbinu za ziada zitakazoweza kuimaliza Yanga.

Huku Yanga nao wakiwa wamezinduka kutoka kupata ushindi wa kubahatisha mpaka ushindi wa uhakika.
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Kuziona Simba na Yanga jumamosi Tshs.10000 uwanja wa Uhuru"

Back To Top