Millionaire  Ads

Samatta kibaruani leo Belgium - Pro League




KRC Genk leo inashuka katika dimba lake la nyumbani la Luminus Arena kumenyana na timu inayoburuza mkia katika Belgium - Pro League timu iitwayo Royal Excel Mouscron. Mchezo utakaopigwa saa 22:00 majira ya Afrka Mashariki.

Cha kujivunia kwa watanzania ni mchezaji Mbwana Samatta ambae anaiwakilisha vyema Tanzania kimataifa kwani mpka sasa yeye yupo nafasi ya 15 pamoja na kiungo mshambuliaji wa Manchester City Kevin De Bruyne kwa upachikaji mabao katika historia ya KRC Genk kwa kutia kambani jumla ya magoli 17 huku anaeongoza akiwa na magoli 105 ambae anaitwa Jelle Vossen.

Hii ina maana kuwa endapo Samatta atafunga goli tatu leo atakuwa sawasawa na Christian Benteke ambae anakipiga katika klab ya Crystal Palace.
Genk ipo nafasi ya 8 baada ya michezo 23 ikiwa na alama 34, huku kinara wa ligi hiyo Club Brugge ikiwa na alama 49 baada ya michezo 24.

Kilalakheri Samatta katika mafanikio yako Watanzania tupo nyuma yako. 
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk "Samatta kibaruani leo Belgium - Pro League"

Back To Top