Millionaire  Ads

Azam yanasa bonge la kipa kuziba pengo la Manula


Safari ya baadhi ya viongozi wa Azam kwenda Ghana hatimae imezaa matunda baada ya kuizidi ujanja  Hearts of Oak na kumsajili golikipa wa timu ya taifa ya Ghana kwa wachezaji wa ndani Razak Abalora kutoka WAFA SC.

Kipa huyo namba moja wa timu ya WAFA tangu 2016 amekuwa na msimu mzuri baada ya kucheza michezo 22 kati ya michezo hiyo michezo 12 amedaka bila kuruhusu nyavu zake kutikiswa.

Razak alichukua nafasi ya Felix Annan ambae alitolewa kwa mkopo kwenda timu ya Asante Kotoko.

Razak amecheza jumla ya michezo 22 msimu huu na kufanikiwa kuisaidia timu yake ya WAFA kuwa katika nafasi ya pili.

Razak Abalora amesaini mkataba wa miaka mitatu ndani ya Azam na huenda akawa ndie mbadala wa Aish Manula.


Razak Abalora anakamilisha idadi ya makipa 4 ndani Azam mpaka, makipa wengine ni Benedict Haule, Menata Boniphace Pamoja na mkongwe Mwadini Ali 
Millionaire  Ads

Share :

Facebook Twitter Google+ Lintasme

Related Post:

0 Comment untuk " Azam yanasa bonge la kipa kuziba pengo la Manula"

Back To Top